A.MUUNDO WA UTAWALA SHETANI WA SHETANI:WAEFESO 6:10-13.
1.Shetani.
Shetani ni mkuu wa utawala wa giza Biblia ina mwita mfalme wa uwezo waanga.Efeso 2:2.
2.Falme.
Falme ni mashetani wa wakilishi wa utawala wa shteni wanaotawala falme kubwa,kimfano mabara kama vile africa,africa mashariki, ulaya ,asia na nk.
3.Wenyemamlaka.
Wenyemamlaka ni mashetani yanayotawala nchi,kupitia tawala za wanadamu.
4.Wakuu wa giza.
Nimashetani yanayotawala manbo ya giza ya kishetani kimfano,uendelezwaji wa dhambi,umaskini,ujinga na magonjwa.
5.Majeshi ya pepo wabaya.
Yanaitwa majeshi kwasababu yapo mengi na yote hayana kazi moja yanafanya kazi kama vikosi vikosi.Kama vile katika mataifa yetu tunamajeshi yaliyogawanyika katika utendaji tofauti tofauti.
6.Binadamu wanaomtumikia shetani walioingia mkataba au agano na shetani ili kumtumikia.Kama vile wachawi,maajenti nk.
B.SILAHA ZETU ZA KUJIHAMI{KUJILINDA}EFESO 6:10-18.
1.Chepeo ya wokovu{kofia}kolosai 1:13.
Chepeo ilikuwa silaha yaani kofia ya chuma iliyovaliwa na askari wa kirumi kuhifadhi kichwa na mashambulizi ya adui.Kiroho chepeo ya wokovu,hulinda akili zetu kutokana na mashambulizi ya shetani.{Kujua ukombozi wako katika Kristo ni ulinzi}
2.Dirii ya haki kifuani.
Dirii ya haki ili kuwani ni fulana ambazo risasi haiwezi kupenya.{bullet proof vest}
Waamini ambao hawajapata ufahamu wa haki ya Kristo wameacha roho zao wazi kwa ajili ya kushindwa.
Tumepewa haki ya Yesu kama zawadi sio kwa kustahili kwetu bali kwa neema yake tu.
Sasa tunao wajibu wa kuishi katika haki kwa kutii neno la Mungu.2Kor.5:21.Nikama mfano raia wa nchi
asiyejua haki zake kama raia nilahisi kupoteza hazako za msingi.Mafundisho mengi leo kuhusu kuvunjiwa laana na kufanyiwa maombi ya ukombozi,mengi ya hayo yamejengwa katika msingi wakutokujua haki zetu ndani ya Kristo kupitia msalaba wake.
3.Kweli viunoni.
Huu ulikuwa ni aina ya mkanda ulifungwa kiunoni,kumsaidia askari mavazi yake kushikamanishwa vizuri na mwili wake na kutokupata shida awapo vitani.Kiroho kweli hii ni tabia ya Mungu ambayo kwa mwamini hufanyika silaha ya kujilinda.Kwasababu adui hana hiyo kweli.Tabia hii inampa mwamini ujasiri wa kukabiliana na kila changamoto katika maisha yake ya imani.
4.Utayari wa injili ya amani.
Utayari wa kutumika hiyo ni silaha kali dhidi ya adui.2Tim 4:2.Unapokuwa unasukumwa sukumwa ili kumtumikia Mungu ujue unapoteza silaha yako dhidi ya adui.Kumbuka shetani na majeshi yake wanafanya kazi kwa bidii usiku na mchana,hapotesi kila fursa inayotokea mbele yake.
5.Ngao ya imani.
Askari wa wakati ule alitumia ngao iliyokuwa ngozi ya mnyama ilitengenezwa kwa mfano wa kama vile ungo ili kuzuia mishale yenye moto isimdhuru mpiganaji.
Imani hufanyika kama uzio wetu wa ulinzi ili kuzima mishale yenye moto.
C.SILAHA ZETU ZA KUSHAMBULIA.
1.Upanga wa Roho{Neno la Mungu}
Tunaweza kufanya kufanya mashambulizi kwa kutumia Neno la Mungu.Ufu.1:16;2:16.Ebr.4:12.Kwa maana hii sasa tunahitaji kulihamisha Neno la Mungu katika kurasa za Biblia na kuliweka ndani ya mioyo yetu,linapotoka ndani ya mioyo yetu kupitia vinywa vyetu huitwa upanga wa Roho.Hii ndiyo silaha ambayo Yesu alitumia ili kumshambulia shetani na hatimaye kumshinda.Math.4:4-11.
2.Jina la Yesu.
Unapompokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako unapewa haki ya uwakili wa kutumia Jina la Yesu.Yoh.16:23-24,Uf.19:13.Kwa kutamka Jina la Yesu unaweza kuharibu kazi zote za shetani.
3.Imani ni silaha ya kujilinda na kushambulia.1Yoh.5:4.Imani ni njia Yetu ya ushindi dhidi ya ya ulimwengu.
4.Kuomba katika roho yaani kunena kwa lugha ni silaha yenye nguvu.
-Ina mjenga mwamini na kumwimalisha
-Maana ya kujenga ni kuinua,kufanya jasiri,kutia nguvu mpya.1Kor.14:4.
5.Sifa.
Sifa ni silaha yenye nguvu dhidi ya adui.
-Sifa humtukuza Mungu
-Sifa humsimamisha na kumzima shetani.Zab.8 na 9.
D.MADHAIFU YA SHETANI.
Ufunguo kwa ushindi katika.
Kujua udhaifu wa adui yako,unakuwa na asilimia kubwa ya kushinda.Shetani huwa anatusoma maeneo yetu ya udhaifu na kushambulia hayo maeneo.
1.Hawezi kutenda kazi katikati ya sifa.Zab.22:3.
Sifa humsimamisha na kumnyamazisha adui.Huteka na kuzishinda ngazi zote za majeshi ya adui.
2.Hawezi kutenda kazi wakati Neno la Mungu limenenwa.Uf.1:16.
3.Hawezi kufanya kazi katika Jina la Yesu kwa sababu limeinuliwa juu ya majina yote.Flp.2:8-11.
4.Hawezi kufanya kazi katika upendo kwa sababu yeye asili yake ni chuki.1Kor.13:13.
5.Hawezikunya kazi katika nuru.Kwasababu yeye ni giza.Zab.119:105.
-Neno liingiapo,huleta nuru au mwangaza.Zab.119:130.
-Unaposimamia Neno la Mungu ni sawa na kama umewasha mwangwa wa taa makali.
6.Hawezi kufanya kazi mahali penye kweli.Neno ndiyo kweli.Yoh.17:17,8:44.
7.Hawezi kufanya kazi wakati Neno la Mungu limepewa mamlaka ya kwanza na ya mwisho katika maisha yako.Yoh.6:68.