Dibaji:Mungu aliwambia Israeli MIMI NI MUNGU NISIYEBADIRIKA.Neno la Mungu huwa halibadiriki ili kuendandana na mazingira.Inamaana mazingira yeyote hatakama nimagumu yakiwa nje ya uwezo wetu kama wanadamu bado hayawezi kulibadiri Neno la Mungu.
Mungu huwa habadiriki ila yeye huwa ana sifa ya kubadilisha.Mungu hadhuriki na chochote kinachoendelea Ulimwenguni huu.
Unaweza kumtegemea Mungu ambaye akisema amesema yeye huwabadilishi kauli yake.Nitofauti na wanadamu ambao leo wanaweza kusema bila kutekeleza walichosema.
Kwakutambua kanuni hizi humfanya mwamini awe na imani isiyoyumba katika Mungu wake.Kwasababu hiyo hupokea mahitaji yake.
A.TAFUTA AHADI KATIKA NENO LA MUNGU KWA KILE UNACHOHITAJI.
Mungu wetu anaishi ndani ya Neno lake na anatenda kazi kwa msingi wa Neno,hakuna njia ya kukutana na Mungu ila ni kwa msingi wa Neno lake.
Kunambo mawili amambayo kamwe hayawezi kubadilishwa au kubadirika.WABRANIA 6:13-18.ZABURI 138:2.
1.Ahadi za Mungu
2.Kiapo cha Mungu
-SHIDA YA WAKRISTO WENGI NI KWAMBA:
1.Hawazijui hizo ahadi
2.Hawaamini hata wanapozijua
3.Wanakaza macho sana kwa shetani na yale anayosema
B.LIAMINI NENO LA MUNGU.
TITO 1:2;HESABU 23:19.Kwasababu Mungu hawezi kusema uongo,anachosema kwako atafanya.
Nilini na kwa namna gani hilo huwajibikinalo.Wewe unawajibika na kumwamini,kuwa hawezi kusema uongo.
1.Wewe unawajibika alichosema nini kisha..
2.Uwe na uhakika wa ndani kabisa kuwa hawezi kudanganya.Mashaka ni kikwazo kikubwa cha kupokea kutoka kwa Mungu.Mk.9:23.
C.USIFIKIRI HALI ZINAZOONEKANA KUPINGANA.IIKor.4:18.
Yakitambo=ya muda tu yaani siyoyakudumu.Kwa lugha nyingine mambo yenyeuwezekano wa kubadirika.Chochote unachokiona kwa macho yako hicho si chakudumu,kipo katika hali ya kubadirika.
Badilisha mtazamo wako juu ya matatizo,majaribu ya napokuja Mungu pia huja kwa msaada wake.
Mf.Lk.8:41-50.Ukisoma Maandiko haya utaona hapa kuwa mazingira yaliyopingana kabisa, lakini bado Mungu alifanya muujiza.
Angalia jawabu la tatizo badala ya kutafakari tatizo lenyewe.IIFalm 6:8-16.
Lione Neno kama linakidhi kikamilifu kukuvusha kwenye tatizo hilo.
1.Ulitambue tatizo
2.Usitafakari wala usiendelee kuliangalia
3.Usiendelee kulizungumuzia.Kuna baadhi ya watu hata wakisha mwomba Mungu bado wanakuwa wakizungumuzia tatizo hilo kila wanapokwenda.
4.Nenda kwenye Neno la Mungu ambalo imani yako hutokea.
5.Jibu hilotatizo ukisimama katika Neno la Mungu.Mk.11:23.Mlima utaondoka kwa kuumbia sio kwa kuutazama tu na kusikitika.
6.Ona yasiyoonekana kwa jicho la IMANI.Imani ni jicho la imani kuona yale yasiyoonekena kwa macho ya kimwili.
D.MSIFU MUNGU KWA AJILI YA JIBU.ZAB.119:89.ZAB.150:1.
Imba kwa imani msifu Mungu kwa jibu hata kama hujaliona kwa macho ya kimwili.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni