Jumamosi, 2 Agosti 2014

kupitia uwanafunzi katika kristo tunamjua Mungu:

Mungu hujidhihirisha kupitia neno lake tu.Wala hatuna jinsi nyingine ya kumfahamu na kumjua Mungu nje ya neno lake hivyo inatupasa kujifunza sana neno lake.Wote waliofanikiwa kuishi na kutembea na Mungu katika maisha yao walikuwa na wanaendelea kuwa wanafunzi wazuri,uwanafunzi hauna kikomo kwani kamwe hatutafikia kikomo cha kumjua Mungu.Berea christian centre tunaamini juu ya uwanafunzi,tunauishi uwanafunzi kwa neno la Mungu na tumekuwa tukikutana na Mungu kwa jinsi ya kipekee sana.Blog hii itakusaidia kukusogeza karibu na Mungu kwa kukupatia mafundisho mbalimbali ya biblia katika nyanja tofautitofauti za maisha yako ya kiroho,kumbuka Mungu anakupenda sana na ana mpango na wewe,sasa ili kukamilisha kusudi la kimungu maishani mwako ni lazima ujifunze.

ZINGATIA:   kama huna mahusiano mazuri na yesu rudia maneno haya chini kwa kuyasoma ........

"Bwana yesu mimi ni mdhambi,ninakuja kwako kuanzia hivi sasa,unisamehe dhambi zangu zote,futa jina langu katika kitabu cha hukumu,andika jina
langu katika kitabu cha uzima wa milele,okoa roho yangu,nafsi na mwili wangu,nifanye kuwa mwanao kuanzia saa hii" 

Baada ya kuyasema maneno hayo kwa dhati na kumaanisha kuachana na maisha ya dhambi unakuwa umeingia katika ufalme wa bwana wetu yesu na umekuwa mtoto wa Mungu.
Beroya itakupatia mtiririko wa masomo ya siku,wiki,mwezi,mwaka.Mafundisho mbalimbali kama ya ndoa,vijana,uchumi na mengineyo mengi ya kiroho.Kwa muda mrefu kumekuwa na milipuko ya mafundisho yasiyo sahihi kiasi cha kuwapelekea watu kushindwa kujisimamia wanapokutana na matatizo maishani.Dawa ya matatizo yote inapatikana katika neno la Mungu lilobeba pumzi ya uhai wa kimungu.
www.facebook.com